Wanahabari wapekuzi wa Afrika wanafanya kazi muhimu ya kutoa maelezo na ufafanuzi wa pandemia ya kirusi cha korona inayokua barani, na kuziwajibisha serikali. Makala za upekuzi zimezindua baadhi ya serikali zilizokuwa zimezubaa katika utayari wake kwa ajili ya kirusi cha korona. Kadhalika, makala za upekuzi za hivi karibuni zimezindua utumizi mbaya wa fedha kupitia tiba bandia na wanakandarasi wenye hila.
Kiswahili
Uanahabari wa Upekuzi: Jinsi ya Kuielezea Sanaa Hii
|
Ijapokuwa maelezo ya uanahabari wa upekuzi hutofautiana, kuna makubaliano mapana miongoni mwa makundi ya kitaaluma ya uanahabari kuhusu nguzo zake muhimu: hufuata mfumo maalum, huwa na kina, hutegemea utafiti asilia na uandishi wa habari ambao mara nyingi huhusisha ufichuzi wa siri. Kwa wengine, upekuzi aghalabu huhusisha matumizi mengi ya data na rekodi za taarifa za umma, huku ukiangazia haki ya kijamii na uwajibikaji.
Kiswahili
GIJN Africa: Ufadhili wa Kifedha
|
Uanahabari wa upekuzi siku zote umekuwa wenye gharama kubwa. Huku tasnia hii ikizidi kukumbwa na hali ngumu ya kiuchumi, mashirika mengi ya habari ya faida yamekoma kutengea upekuzi wa habari fedha nyingi kama ilivyokuwa hapo kabla.
Kiswahili
GIJN Africa: Usalama na Ulinzi Barani Afrika
|
Katika asili yake yenyewe, uanahabari wa upekuzi ni tasnia yenye hatari ambayo huwaweka wanahabari na wahariri kwenye hatari mtandaoni na nje ya mtandao. Wanahabari wanaochimbua maasi ya maafisa wa serikali fisadi na maajenti wa ulinzi wakandamizaji hukabiliwa na vitisho vinavyolenga kuwakomesha au kudhibiti vyombo vya habari vyao hali kadhalika.
Kiswahili
COVID-19: Ushauri wa Kitaalamu Kuhusu Mitazamo ya Kuchunguzia
|
Kufuatia mikakati isiyo ya kawaida inayochukuliwa ili kukabili mlipuko wa kirusi cha korona, kazi ya wanahabari wapekuzi ya kuchunguza matumizi mabaya ya mamlaka na unyanyasaji wa wanyonge imekuwa muhimu zaidi wakati huu. Katika janga hili linaloenea kwa kasi, wanahabari wapekuzi wanapaswa kuanzia wapi?
Kiswahili
GIJN Africa: Kupata Rekodi za Umma
|
Katika mataifa mengi ya kusini mwa jangwa la Sahara, kupata habari za umma ni jinamizi mpaka leo. Hii ni kwa sababu hakuna sheria zinazofadhili maombi ya kupata rekodi za wanahabari, au zinazowashinikiza maafisa wa serikali kusalimisha rekodi za umma zinazomilikiwa na serikali.
Kiswahili
Jinsi ICIR Nchini Nigeria Linavyoshinikiza Uwajibikaji Katika Kukabili Kirusi cha Korona
|
Shirika moja la uanahabari wa upekuzi lisilo la faida nchini Nigeria, International Centre for Investigative Reporting (ICIR), limepitiliza katika mbinu zake za kuchunguza jinsi Nigeria inavyokabiliana na kirusi cha korona. Kwenye mahojiano na mhariri wa GIJN Africa Benon Herbert Oluka, mkurugenzi mkuu wa ICIR Dayo Aiyetan anaeleza kazi wanayofanya.
covid-19
Mwongozo Kwa Wanahabari Wanaoripoti Kuhusu COVID-19
|
English
Kirusi kipya cha korona kimekuwa taarifa kuu zaidi duniani. Kufikia sasa kimesambaa katika mataifa zaidi ya 100, kuwaua watu 4,262 na kuwaambukiza zaidi ya 118,101.